Mimi… (Jina) mkosefu, maskini mwenye imani haba, siku ya leo ninafanya tena upya ahadi zangu za Ubatizo, nikijiaminisha katika mikono yako, Pa Moyo Safi wa Bikira Maria. Ninamkataa shetani daima na mambo yake yote na kazi zake na ninajitolea kabisa kwa Yesu Kristo, hekima ya umwilisho, kwa kuubeba msalaba wangu na kumfuata siku zote za maisha yangu. Na nitakuw mwaminifu kwake zaidi tangu sasa, kuliko nilivyofanya zamani.
Mbele ya Jeshi lote la mbinguni, leo nimekuchagua wewe uwe Mama na msaada wangu. Nitajitoa na kujiweka wakfu kabisa kwako, kama mtumwa wako, mwili na roho yangu, mema yangu, ya ndani na nje, na hata yale matend mema, ya zamani, ya sasa na wakati ujao; nikikuachia kila kitu hata haki zangu zote na yote yaliyo yangu bila kubagua; uyatumie yote upendavyo, kwa ajili ya utukufu zaidi wa Mungu, kwa sasa na milele. Amina.

Leave a comment